Na Deogratius Temba
SIKU mbili baada ya kampuni ya kusambaza mafuta ya Uingereza (BP), kutangaza kutaka kuuza hisa zake zilizopo Tanzania, serikali imesema itakuwa tayari kuzinunua mara kampuni hiyo itakapoamua kufanya hivyo.
Serikali inamiliki asilimia 50 ya hisa za kampuni ya BP Tanzania Limited, na kampuni hiyo yenye makao yake makuu nchini Uingereza ina asilimia 50, ambazo kwa sasa imatangaza kuziuza.
Akijibu swali la waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam, Waziri wa Nishati na Madini Wiliam Ngeleja, alisema serikali inasubiri wakati utakapofika BP wakitaka kuuza hisa zake inazomiliki itazinunua na kama kutakuwa na ulazima jina la BP litabadilika baada ya kuachia hiza zake.
“Serikali imepokea taarifa kutoka BP, kuwa wanania ya kuuza hiza zao, lakini hawajesema kama ni lini. Wameona soko lao hapa labda siyo nzuri na wameamua kujizatiti katika nchi nyingine, hasa katika kipindi hiki cha ushindani ya kibiashara,” alisema na kuongeza:
“Hakuna mwekezaji kutoka nje atakaye kuja kuichukua kampuni hiyo bila kupitishwa na serikali, na baada ya hisa kuuzwa kuna uwezekano wa jina kubadilika,’alisema Ngeleja.
Waziri Ngeleja alisema mara BP itakapofika nchini kwaajili ya kufanya mashauriano na serikali ofisi yake itaishirikisha wizara za fedha, na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali ili mkataba wao uweze kuvunjwa vizuri
Alisema BP haitaweza kuuza hiza hizo bila kuipa serikali taarifa kwani ndiye mbia mwenza, na serikali inapaswa kupewa kipaumbele katika ununuzi wa hiza.
Kampuni hiyo kubwa ya mafuta imekuwa ikifanya biashara hiyo kwa zaidi ya karne moja nchini imetangaza kuondoa hiza zake katika nchi kadhaa za Afrika kwa sababu za kibiashara.
Mtendaji Mkuu wa BP Afrika, Sipho Maseko, alitangaza siku ya Jumanne kuwa uamuzi wa kuondoa hiza zake Tanzania umafikiwa baada ya kufanyika kwa mapitio ya upembuzi yakinifu wa kibiashara na kuona kuwa nchi hiyo iweke nguvu zaidi katika nchi za Angola, Msumbiji, Afrika ya Kusini, Misri, Algeria, na Libya.
Ukiacha Afrika ya Kusini nchi nyingine ambazo BP ameamua kubaki ni zile zinazozalisha mafuta . Pia mbali na Tanzania BP imejiondoa kuendesha biashara katika nchi za Namibia, Malawi, Zambia na Botswana.
Waziri Ngeleja alisema kununua hiza hizo kutakuwa ni uamuzi wa haraka wa serikali.
Mwisho
Elimu ni kujifunza! Tunajifunza kwa kusoma! Karibu katika Blog hii ili tufundishane na kubadilishana Mawazo
Popular Posts
-
*alikubali kushindwa kwa siasa za Kijamaa *hakujilimbikizia mali Na Deogratius Temba WAKATI taifa linaadhimisha miaka 10 ya kifo cha mwasisi...
-
Na Deogratius Temba KWARESMA ni kipindi cha mfungo kwa waumini Wakatoliki. Mfungo huu ni wa siku hamsini. Kipindi hiki kinaanza na ibada ya ...
-
KAMPALA Uganda Dawa za kupunguza makali ya virusi vya ugonjwa wa Ukimwi ARVs, zikitumika sambasamba na dawa mseto aina ya (co-Trimoxazole), ...
-
Na Deogratius Temba. NI takribani miaka mitano tangu ililipo ibuika suala la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, iliyokwapua sh. Bilioni ...
-
*Ilizamishwa ziwani na wakaoloni baadaye ikafufuka *Ina Umri wa miaka 98, mwaka 2013 itavunja rekodi ya dunia Na Deogratius Temba MV Liemba ...
-
Na Deogratius Temba SERIKALI imesema makazi ya Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Mzee Abdul Jumbe, yaliyoko Kigambo...
-
*Ni ajali iliyoweka historia kwa kuua *Bado usalama wa ziwani haujaimarika Na Deogratius Temba MEI 21, mwaka huu taifa limetimiza miaka 14 ...
-
, tutaendanayo mpaka uchaguzi Mkuu 2010 Na Deogratius Temba MWISHONI mwa wiki iliyopita Jumuiya ya wanawake wa Chama Cha mapinduzi, (CCM), w...
-
TITLE OF THE PROJECT The effect of Water Conflict between Investor of VASSO Estate and Villagers in Kibosho Dakau, Moshi Kilimanjaro JOURNAL...
-
Taasisi ya mafunzo ya Jinsia (GTI) inayomilikiwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) inaendelea na mafunzo ya kuwanoa wanaharakati kuanzia ...
No comments:
Post a Comment