Popular Posts

Friday, September 9, 2011

DPP umemskia Manji? Anawaweza kuwa shahidi Muhimu

Na Deogratius Temba.
NI takribani miaka mitano tangu ililipo ibuika suala la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, iliyokwapua sh. Bilioni 40 kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Kwa kipindi chote hicho, serikali imekuwa na kigugumizi cha kukataa kumtaja mmiliki halali wa kampuni hiyo, licha ya mamlaka ya usajili wa makampuni (BRELA) kutaja majina ya wamiliki ambao hata hivyo Watanzania waamini kuwa ni wamiliki ‘feki’.
Kwa muda mrefu Watanzania wamkuwa na uchungu dhidi ya wizi wa rasilimali zao na watu wachache kuliibia taifa hili na kunufaika wao binafsi wakati mamilioni ya Wananchi wakitaabika na umasikini wa kutupwa. Watanzania wameitaka serikali kumtaja mmiliki halali wa Kagoda na mahusiano yake na Chama Cha Mapinduzi(CCM), lakini imekaa kimya. Mfanya biashara Yusuf Manji, anaweza kuwa shahidi muhimu sana wa kesi hii, akatueleza mahali ofisi za Kagoda zilipo na wamiliki wake na aliyempeleka Kagoda kufanya nao mikataba.
Kuna usemi usemao “za Mwizi ni arobaini” sasa zimefika, kila kitu dhidi ya Kagoda kitaanikwa na ulimwengu utaujua ukweli na nchi yetu itakuwa huru.
Bunge limelalamikia mara kadhaa juu ya mmiliki wa Kagoda lakini serikali haikutaka kumtaja mmiliki, serikali imetakiwa kuwataja hadharani walioiba fedha za EPA kupitia Kagoda lakini imekataa, lakini nchi hii ilivyo na za mwizi zinavyotimia, wanajitaja wenyewe na wanajianika waziwazi. Tunasubiri kuyaona mengi zaidi. Manji amejua kuwa maji yamemfika shingoni, pamoja na usiri wa serikali na vyombo vya dola kutomtaja, lakini yeye anaona hali yake inazidi kuwa mbaya kwasababu anashambuliwa na ameamua kukiri kuwa amekwapua fedha za EPA. Hii ni hatua nzuri.
Na hii ni ngumu ya umma imezaa matunda, lamsingi ni kwamba watanzania wazalendo hawatachoka kurusha mawe kwenye mapango walimojificha wahujumu uchumi hadi wachomoke wenyewe.
Tunajiuliza ni kwanini serikali imeendelea kuwa na Manji karibu kama rafiki wao na mfadhili wa CCM wakati moja ya kampuni zake kama hii ya Quality Finance Cooperation Limited imechukua fedha za wananchi na kukaa nazo bila kulipa riba? Je huu sio wizi wa rasilimali za wananchi masikini? Je kama serikali isingeshinikizwa na vyombo vya habari na wanaharakati mbalimbali, juu ya wizi wa EPA Manji angerejesha fedha hizo?
Manji mwenyewe amekuwa msiri kwa kipindi kirefu, kama kweli angekuwa mzalendo na mwananchi mwenye uchungu na taifa hili angekuwa amejitokeza tangu awali na kutangaza kuwa kampuni yake ni moja ya waliokopa Kagoda na kueleza ukweli juu ya utapeli aliofanyiwa na KAGODA, lakini hajawahi kujitokeza waziwazi hadi alipotajwa mara kadhaa kuwa yeye ni mmiliki. Sasa anajitoa.
Kwa mara ya kwanza, pamoja na kutajwa na wanasiasa kuwa ni mmoja wa waliokwapua fedha hizo, uhusika wa Manji kwenye EPA ulianza kuonekana na kudhibitika kwenye vielelezo vya ushahidi kwenye kesi yake ya madai ya shilingi 1, dhidi yake na Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Reginald Mengi. Watanzania wanaotafakari kwa haraka na kupata majibu waliliona hilo na kulihitimisha. Lakini Mahakama haikutaka vielelezo hivyo viwe wazi.
Kitu cha kujiuliza kwa kipindi chote hicho, pamoja na kushinikizwa serikali imegoma kabisa kuwataja Manji na washirika wake wengine kuwa ni watuhumiwa wa EPA, imegoma hata kuwataja waliorudisha fedha hadi wanajitaja wenyewe. Hii ndio serikali tulioiweka madarakani, tunajidai kuwa eti ni serikali ya demokrasia, uwazi, na ukweli. Je kweli hapa kuna utawala bora?
Kwa hili la kumficha Manji hadi anajitokeza mwenyewe nidhahiri kuwa nchi yetu ipo mikononi mwa kundi la watu wachache na serikali haiwawezi. Tusipoteze muda kumjadaili Manji na kampuni zake ila atusaidie ushaidi. Akihojiwa kiukweli kama vyombo vyetu vya dola vipo huru basi anaweza kupelekewa mahakamani.
Na kama Kagoda ni mali ya serikali basi tuelezwe ukweli, na kama ni CCM tuambiwe kwasababu sasa Manji ametangaza mgogoro na Kagoda na anawadai ina maana anaweza kulipwa kwa fedha za walipa kodi. Wakati waliozitumia fedha hizo ni wengine. Tunataka kupata mwongozo wa wazi, na serikali ivunje ulimya kwenye suala la Kagoda.
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini(DPP) analojukumu la kutekeleza sheria na kuonesha dhana ya utawala wa kisheria hapa nchini kwa kumkamata Manji na kumhoji, na sio kumhoji tu atoe ushahidi muhimu kabisa juu ya kampuni ya Kagoda, kama hili halitafanyika tuamini kuwa Kagoda ndio imeiingiza serikalki madarakani na siku ikitajwa serikkali itavunjika.
Pamoja na kuwa Manji analalamika nay eye ameshatuibia kwa kumiliki fedha za walipa kodi masikin wa taifa hili bila huruma huku akishuhudia wazee wetu wakifariki kwa kukosa asipirini hospitalini, kukosekana kwa maji safi ya kunywa na zahanati wakati yeye anafaidi faida lukuki kwa mabilioni yetu, atoe ushaidi halisi wa kumtaja mmiliki halali wa Kagoda.
Pamoja na kuwa Manji hajataja kiasi hali cha fedha alichochukua Kagoda asiendelee kulalamika kuwa amepata hasara kwa fedha (mabilioni) ambayo amekaa nayo miaka mitatu. (2005-2008) huwezi kukaa na mabilioni ya mtu kwa kipindi hicho ukawa huna faida.
Pia Manji arudishe sehemu ya faida kwa wananchi kwa kujenga zahanati vijijini na dawa ili watanzania wamsmehe.
DPP anatakiwa kuheshimu katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumkamata Manji ali amsaidie usahhidi muhimu. Kama DPP atashindwa kuwapeleka mhakamani wamiliki wa Kagoda kwa atakuwa ameshiriki kuwaibia watanzania rasilimali zao na atakuwa amevunja katiba inayompa mamlaka ya kumshitaki, kumkamata mtuhumiwa na kumfungulia mashataka pale anapojiridhisha kuwa amehusika na kosa.
Kila la heri na jumapili njema!

: jamii
HIKI NDIYO KIJIJI KILICHOCHOMWA MOTO HUKO TABORA
Mkazi wa Kitongoji cha Luganjo Mtoni katika Tarafa ya Usinge mkoani Tabora, Bahati Hussein (kulia), akiwa amekaa na familia yake nje ya mabaki ya nyumba yake, baada ya kuchomwa moto na askari wa wanyamapori na polisi agosti 15 mwaka huu kwa madai ya kujenga katika hifadhi. Nyumba 317 zilichomwa na watu 773 hawana mahali pa kuishi wanaishi vichakani.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Mgusa Maduhu (kulia) akiwa na familia yake baada ya nyumba yake kuchomwa moto.
Wakazi wa kijiji hicho wakiwaonesha mabaki ya baiskeli iliyoungua moto katika tukio hilo.
watoto wakicheza vichakani katika eneo la wazi walipopewa hifadhi na serikali ya kijiji.
Mama Mlemavu Magreth Jonas akilia wakati akihojiwa na waandishi wa habari hawapo pichani.
Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho waliochomewa nyumba zao.
Mama akipika nje baada ya nyumba yake kuchomwa moto huku watoto wake wakisubiri chakula kiive tayari kwa mlo wa mchana.

Mkazi wa kijiji hicho Elia Mrisho akionesha mafuvu ya nguruwe wake waliochomwa moto. Nguruwe 26 waliteketea.
muandishi: JOHN BUKUKU tarehe: 8/24/2011 0 maoni
Labels: jamii

Magunzo ya uwezeshaji ngazi ya kitaifa

Taasisi ya mafunzo ya Jinsia (GTI) inayomilikiwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) inaendelea na mafunzo ya kuwanoa wanaharakati kuanzia ngazi ya kijamii, hadi kitaifa kwa kuwajengea uwezo wawezeshaji wa ngazi ya kitaifa ili waweze kufika vijijini.
GTI ambacho ni chuo pekee kinachotoa mafunzo ya Jinsia nchini, kilianza kama program za TGNP wakati shirika lilipoanzishwa mwaka 1993, na mwaka 2008 GTI imeandikishwa kama Chuo au taasisi ya mafunzo katika baraza la elilimu ya ufundi (NACTE).
Wakati harakati zikiendelea GTI kimeweza kutoa mafunzo na kuandaa mitaala katika ngazi ya 1,2,3,4 na 6, na kupata kibali cha kutoa cheti na stashahada(Diploma).
Akifungua mafunzo ya wawezeshaji ngazi ya kitaifa yalkiyopfanyika kuanzia …… katika Mambibo dare s salaam, Mkurugenzi wa GTI, Dk.Diana Mwiru, amesema Watanzania wote hawatatulia hadi ukomboziz wa mwanamke kimapinduzi ufanikiwe na taifa likubali mabadiliko hayo “ TGNP tunatambua kuwa suala la vuguvugu na mapambanao dhidi ya ukombozi wa mwanamke na usawa wa kijinsia hapa nchini sio letu pekee. Tunajikita zaidi kuwa chachu ya mabadiliko kwa kuwajengea watu wengi uwezo ili waweze kufanya maamuzi yao wenyewe”Amesema Dk. Diana
Kwa mujibu wa Dk. Diana Ni jukumu la TGNP kujenga uwezo kwa watu wa ngazi zote hatua inayoifanya taasisi hiyo kuwa na jukumu kubwa la kutekeleza mipango yake ya kuibadilisha jamii na kuifanya ikubali mabadiliko hasa yale ya kimapinduzi.
“katika kutekeleza hilo hatuwezi tukiwa na watu wachache kwani kidole kimoja hakivunji chawa; harakati zinahitaji nguvu ya pamoja ili kupaaza sauti kwa nguvu kupigania haki za wanyomnge.
Kwa upande wa washiriki wa mafunzo, walitakiwa kuheshimu muda wanapokuwa katika mafunzo,kujiweka tayari kupokea, kwani malengo ya mafunzo hayo yalikuwa ni kuwajengea washiriki uelewa na maarifa zaidi katika kuhoji na kufanya uraghbishi katika ngazi ya kijamii.
Pia mafunzo haya yamelenga kuwajengea uwezo wawezeshaji kuelewa dhana na muktadha wa kimapinduzi ikiwemo kukuza namna ya kuwa waraghibishi zaidi. Kutaka kujenga vuguvugu la kimapinduzi na kukuza namna ya kuw waraghibishi zaidi.

Kilimo kwanza kinawanyonya wanyonge –Bashiru Ally

TGNP yazindua hambuzi wa sera ya Kilimo kwanza,ajira na maisha endelevu
Katika kuhakikisha Tanzania inakuwa taifa lenye kufuata usawa wa kijinsia katika umiliki wa rasilimali zake, Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) mwaka huu umefanya uchambuzi wa kina kupitia na kutoa maoni yenye mtazamo wa Kijinsia sera ya KILIMO KWANZA, na Ajira, maisha endelevu na biashara.
Muadhiri mwandamizi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa TGNP, Bashiru Ally, amesema katika uchambuzi huo kuwa kutokana na serikali kudhararu na kukipouuza KILIMO, kumesababisha kupotea kwa ajira na watanznaia kugeuzwa kuwa watumwamanamba na kunyanyaswa na wawekezaji.
“Hili ni suala la mapambano kuhusu utu na uhai wetu,adhari za kupoteza ajira ni kugeuzwa kuwa watumwa, na kudharauliwa na wawekezaji. Tujiulize nani atatuondoa ktuika kwenye minyororo hii? “ amesema Bashiru.
Mataifa ya ulaya na amerika yamefilisika kutokana na mitikisiko ya kifedha, yamehamia Afrika kuongeza uporaji ili kukuza mitaji yao. “Tuimarishe mijadala ya kijamii vijijini bila kuogopa”
Bashiru ameishauri jamii kujitahidi kupata taarifa kwa kushiriki katika mijadala ya pampoja vijijini au katika mitaa yao, ili kupta taarifa za kitu ganio kinaendela katika taifa lao, na watafute nafasi ya kutoa maoni yao. “Kutokuwa na taairfa za kutosha kunaweza kukusababisha kukusa fursa zilizopo katika nchi yako na ukakosa kukubali au kukosoa”
Mchambuzi na mwanaharakati wa Chuo Kikuu cha Mzumbe,Profesa Aida Isinika, akichamnbua sera ya kilimo anasema: “ uwekezaji wa serikali kwenye kilimo ni mdogo sana ni wa manenoi kuliko matendo kwani kasi ya kiutendaji katika kupunguza umasikini ni ndogo. Ni lazima kuongeza utendaji na kuweka mikakati endelevu inayotekelezeka”
Katika sekta binafsi fursa zipo kwenye mikopo, wkati dirisha dogo linalotajwa kuwa lipo katika benki ya rasilimali Tanzania(TIB) mkulima mdogo hawezi kwenda kukopa hapo kwani kiasi cha kukopa ni kuanzia Sh. Milioni 100 hadi Bilioni 1, na uweke amana ambazo mkulima mdogo hawezi kumiliki kama hati za nyumba, mashamba makubwa na vitu vingine.
Katika mchakato huu, KILIMO kwanza kimeonekana kama ni ajenda ya watu wakubwa wenye mitaji kwasababu, nguzo ya kwanza ya sera hiyo ni kuleta mapinduzi katika kilimo na kusababisha mapinduzi ya kijani. Wakati miundombinu yta barabra ni mibovu, kutoka shambani ili kufikia masoko ni tataizo kubwa.
Katika uchambuzi huo, Profesa Isinika anaainisha kuwa, kuna umuhimu mkubwa wa kilimo nchini Tanznaia hasa kile cha wazalishaji wadogo. asilimia 74 ya ajira zote zinatokana na kilimo,asilimia 95 ya chakula kinachotumia hapa nchni kinatoakna na wakulima wadogo,asilimia 30 ya biadhaa zinazouzwa nchi za nje zinataka kwao, asilimia 65 ya malighafiu zinazotumika viwandani hapa nchini.
Asilimia 9o ya chakula kinachozalishwa kinatokana na wakulima wadogo wakati 99 ya ardhi inayolimwa inalimwa na wakulima wadogo wanawake wakiwa ni nusu ya wakulima wadogo.

Pia katika kuzalisha, KILIMO KWANZA kinataka kuwepo na viwanda vya mazao, wakati taifa linatatizo kubwa la upoatikanaji wa umeme wa uhakika, mikoa mingi ay wilaya zinazolima kama vile Namtumbo na Songea Vijijini hawana nishati ya umeme ya Gridi ya Taifa, kwani wakati mafuta ya mitambo yakipanda bei kila mara wao bado wanatumia umeme wa majenereta yanayotumia mafuta
Mwanaharakati mwingine Amina Mcheka amesema kuwa sera ya kilimo kwanza haiajamsaidia mkulima wa chini, maeneo ya kulima yenye maporio yameachwa bila kuwagawia wananchi, wakulima amabo wanamiliki ardhi nzuri wananyang’anywa na kupewa wawekezaji.
Marjorne Mbilinyi anasema kuwa serikali inatakiwa kuelewa kuwa ajira ni kupaumbele kwani hatuwezi kuzungumza habari ya kupunguza umasikini bila kuzngumzia ajira. “katika kilimo wafanyabiashara wakubwa wamekuja na mbegu zilizopunguzwa vinasaba, wafanyabiasahara wa makampuni makubwa wamegeuka kuwa wauaza mbolea, pembejeo za kilimo, dawa; hii inaonesha jinsi ambavyo mfumo wa ubeparfi umeingia kwenye kilimo na kusambabsha tabaka kubwa” anasemna Marjorine
Tom Laizer kutoka Muungano wa Vikundi vya wakulima(MVIWATA) Morogoro anasema kuwa mapngao wa kilimo kwanza umezinduliwa bila kuwaeleza wananchi jinsi ya kupoata taarifa na fursa za kilimo. Wanaopata ni wawekezaji pekee.amesmea neon mapinduzi ya kijani ni neno ngumu ambalo sii kila mkulima anaweza kulizungumzia. “ Kilimo kwanza ni mpango wa kuwafukuza wakulima wadogo masikini kutoka kwenye ardhi yao na kuwapatia wageni, kwani kwa miaka ya hivi karibuni inaonekana kuwa migogoro ya ardhi inaongezeka.

Kilimo kwanza kinawanyonya wanyonge –Bashiru Ally

TGNP yazindua hambuzi wa sera ya Kilimo kwanza,ajira na maisha endelevu
Katika kuhakikisha Tanzania inakuwa taifa lenye kufuata usawa wa kijinsia katika umiliki wa rasilimali zake, Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) mwaka huu umefanya uchambuzi wa kina kupitia na kutoa maoni yenye mtazamo wa Kijinsia sera ya KILIMO KWANZA, na Ajira, maisha endelevu na biashara.
Muadhiri mwandamizi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa TGNP, Bashiru Ally, amesema katika uchambuzi huo kuwa kutokana na serikali kudhararu na kukipouuza KILIMO, kumesababisha kupotea kwa ajira na watanznaia kugeuzwa kuwa watumwamanamba na kunyanyaswa na wawekezaji.
“Hili ni suala la mapambano kuhusu utu na uhai wetu,adhari za kupoteza ajira ni kugeuzwa kuwa watumwa, na kudharauliwa na wawekezaji. Tujiulize nani atatuondoa ktuika kwenye minyororo hii? “ amesema Bashiru.
Mataifa ya ulaya na amerika yamefilisika kutokana na mitikisiko ya kifedha, yamehamia Afrika kuongeza uporaji ili kukuza mitaji yao. “Tuimarishe mijadala ya kijamii vijijini bila kuogopa”
Bashiru ameishauri jamii kujitahidi kupata taarifa kwa kushiriki katika mijadala ya pampoja vijijini au katika mitaa yao, ili kupta taarifa za kitu ganio kinaendela katika taifa lao, na watafute nafasi ya kutoa maoni yao. “Kutokuwa na taairfa za kutosha kunaweza kukusababisha kukusa fursa zilizopo katika nchi yako na ukakosa kukubali au kukosoa”
Mchambuzi na mwanaharakati wa Chuo Kikuu cha Mzumbe,Profesa Aida Isinika, akichamnbua sera ya kilimo anasema: “ uwekezaji wa serikali kwenye kilimo ni mdogo sana ni wa manenoi kuliko matendo kwani kasi ya kiutendaji katika kupunguza umasikini ni ndogo. Ni lazima kuongeza utendaji na kuweka mikakati endelevu inayotekelezeka”
Katika sekta binafsi fursa zipo kwenye mikopo, wkati dirisha dogo linalotajwa kuwa lipo katika benki ya rasilimali Tanzania(TIB) mkulima mdogo hawezi kwenda kukopa hapo kwani kiasi cha kukopa ni kuanzia Sh. Milioni 100 hadi Bilioni 1, na uweke amana ambazo mkulima mdogo hawezi kumiliki kama hati za nyumba, mashamba makubwa na vitu vingine.
Katika mchakato huu, KILIMO kwanza kimeonekana kama ni ajenda ya watu wakubwa wenye mitaji kwasababu, nguzo ya kwanza ya sera hiyo ni kuleta mapinduzi katika kilimo na kusababisha mapinduzi ya kijani. Wakati miundombinu yta barabra ni mibovu, kutoka shambani ili kufikia masoko ni tataizo kubwa.
Katika uchambuzi huo, Profesa Isinika anaainisha kuwa, kuna umuhimu mkubwa wa kilimo nchini Tanznaia hasa kile cha wazalishaji wadogo. asilimia 74 ya ajira zote zinatokana na kilimo,asilimia 95 ya chakula kinachotumia hapa nchni kinatoakna na wakulima wadogo,asilimia 30 ya biadhaa zinazouzwa nchi za nje zinataka kwao, asilimia 65 ya malighafiu zinazotumika viwandani hapa nchini.
Asilimia 9o ya chakula kinachozalishwa kinatokana na wakulima wadogo wakati 99 ya ardhi inayolimwa inalimwa na wakulima wadogo wanawake wakiwa ni nusu ya wakulima wadogo.

Pia katika kuzalisha, KILIMO KWANZA kinataka kuwepo na viwanda vya mazao, wakati taifa linatatizo kubwa la upoatikanaji wa umeme wa uhakika, mikoa mingi ay wilaya zinazolima kama vile Namtumbo na Songea Vijijini hawana nishati ya umeme ya Gridi ya Taifa, kwani wakati mafuta ya mitambo yakipanda bei kila mara wao bado wanatumia umeme wa majenereta yanayotumia mafuta
Mwanaharakati mwingine Amina Mcheka amesema kuwa sera ya kilimo kwanza haiajamsaidia mkulima wa chini, maeneo ya kulima yenye maporio yameachwa bila kuwagawia wananchi, wakulima amabo wanamiliki ardhi nzuri wananyang’anywa na kupewa wawekezaji.
Marjorne Mbilinyi anasema kuwa serikali inatakiwa kuelewa kuwa ajira ni kupaumbele kwani hatuwezi kuzungumza habari ya kupunguza umasikini bila kuzngumzia ajira. “katika kilimo wafanyabiashara wakubwa wamekuja na mbegu zilizopunguzwa vinasaba, wafanyabiasahara wa makampuni makubwa wamegeuka kuwa wauaza mbolea, pembejeo za kilimo, dawa; hii inaonesha jinsi ambavyo mfumo wa ubeparfi umeingia kwenye kilimo na kusambabsha tabaka kubwa” anasemna Marjorine
Tom Laizer kutoka Muungano wa Vikundi vya wakulima(MVIWATA) Morogoro anasema kuwa mapngao wa kilimo kwanza umezinduliwa bila kuwaeleza wananchi jinsi ya kupoata taarifa na fursa za kilimo. Wanaopata ni wawekezaji pekee.amesmea neon mapinduzi ya kijani ni neno ngumu ambalo sii kila mkulima anaweza kulizungumzia. “ Kilimo kwanza ni mpango wa kuwafukuza wakulima wadogo masikini kutoka kwenye ardhi yao na kuwapatia wageni, kwani kwa miaka ya hivi karibuni inaonekana kuwa migogoro ya ardhi inaongezeka.

Kilimo kwanza kinawanyonya wanyonge –Bashiru Ally

TGNP yazindua hambuzi wa sera ya Kilimo kwanza,ajira na maisha endelevu
Katika kuhakikisha Tanzania inakuwa taifa lenye kufuata usawa wa kijinsia katika umiliki wa rasilimali zake, Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) mwaka huu umefanya uchambuzi wa kina kupitia na kutoa maoni yenye mtazamo wa Kijinsia sera ya KILIMO KWANZA, na Ajira, maisha endelevu na biashara.
Muadhiri mwandamizi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa TGNP, Bashiru Ally, amesema katika uchambuzi huo kuwa kutokana na serikali kudhararu na kukipouuza KILIMO, kumesababisha kupotea kwa ajira na watanznaia kugeuzwa kuwa watumwamanamba na kunyanyaswa na wawekezaji.
“Hili ni suala la mapambano kuhusu utu na uhai wetu,adhari za kupoteza ajira ni kugeuzwa kuwa watumwa, na kudharauliwa na wawekezaji. Tujiulize nani atatuondoa ktuika kwenye minyororo hii? “ amesema Bashiru.
Mataifa ya ulaya na amerika yamefilisika kutokana na mitikisiko ya kifedha, yamehamia Afrika kuongeza uporaji ili kukuza mitaji yao. “Tuimarishe mijadala ya kijamii vijijini bila kuogopa”
Bashiru ameishauri jamii kujitahidi kupata taarifa kwa kushiriki katika mijadala ya pampoja vijijini au katika mitaa yao, ili kupta taarifa za kitu ganio kinaendela katika taifa lao, na watafute nafasi ya kutoa maoni yao. “Kutokuwa na taairfa za kutosha kunaweza kukusababisha kukusa fursa zilizopo katika nchi yako na ukakosa kukubali au kukosoa”
Mchambuzi na mwanaharakati wa Chuo Kikuu cha Mzumbe,Profesa Aida Isinika, akichamnbua sera ya kilimo anasema: “ uwekezaji wa serikali kwenye kilimo ni mdogo sana ni wa manenoi kuliko matendo kwani kasi ya kiutendaji katika kupunguza umasikini ni ndogo. Ni lazima kuongeza utendaji na kuweka mikakati endelevu inayotekelezeka”
Katika sekta binafsi fursa zipo kwenye mikopo, wkati dirisha dogo linalotajwa kuwa lipo katika benki ya rasilimali Tanzania(TIB) mkulima mdogo hawezi kwenda kukopa hapo kwani kiasi cha kukopa ni kuanzia Sh. Milioni 100 hadi Bilioni 1, na uweke amana ambazo mkulima mdogo hawezi kumiliki kama hati za nyumba, mashamba makubwa na vitu vingine.
Katika mchakato huu, KILIMO kwanza kimeonekana kama ni ajenda ya watu wakubwa wenye mitaji kwasababu, nguzo ya kwanza ya sera hiyo ni kuleta mapinduzi katika kilimo na kusababisha mapinduzi ya kijani. Wakati miundombinu yta barabra ni mibovu, kutoka shambani ili kufikia masoko ni tataizo kubwa.
Katika uchambuzi huo, Profesa Isinika anaainisha kuwa, kuna umuhimu mkubwa wa kilimo nchini Tanznaia hasa kile cha wazalishaji wadogo. asilimia 74 ya ajira zote zinatokana na kilimo,asilimia 95 ya chakula kinachotumia hapa nchni kinatoakna na wakulima wadogo,asilimia 30 ya biadhaa zinazouzwa nchi za nje zinataka kwao, asilimia 65 ya malighafiu zinazotumika viwandani hapa nchini.
Asilimia 9o ya chakula kinachozalishwa kinatokana na wakulima wadogo wakati 99 ya ardhi inayolimwa inalimwa na wakulima wadogo wanawake wakiwa ni nusu ya wakulima wadogo.

Pia katika kuzalisha, KILIMO KWANZA kinataka kuwepo na viwanda vya mazao, wakati taifa linatatizo kubwa la upoatikanaji wa umeme wa uhakika, mikoa mingi ay wilaya zinazolima kama vile Namtumbo na Songea Vijijini hawana nishati ya umeme ya Gridi ya Taifa, kwani wakati mafuta ya mitambo yakipanda bei kila mara wao bado wanatumia umeme wa majenereta yanayotumia mafuta
Mwanaharakati mwingine Amina Mcheka amesema kuwa sera ya kilimo kwanza haiajamsaidia mkulima wa chini, maeneo ya kulima yenye maporio yameachwa bila kuwagawia wananchi, wakulima amabo wanamiliki ardhi nzuri wananyang’anywa na kupewa wawekezaji.
Marjorne Mbilinyi anasema kuwa serikali inatakiwa kuelewa kuwa ajira ni kupaumbele kwani hatuwezi kuzungumza habari ya kupunguza umasikini bila kuzngumzia ajira. “katika kilimo wafanyabiashara wakubwa wamekuja na mbegu zilizopunguzwa vinasaba, wafanyabiasahara wa makampuni makubwa wamegeuka kuwa wauaza mbolea, pembejeo za kilimo, dawa; hii inaonesha jinsi ambavyo mfumo wa ubeparfi umeingia kwenye kilimo na kusambabsha tabaka kubwa” anasemna Marjorine
Tom Laizer kutoka Muungano wa Vikundi vya wakulima(MVIWATA) Morogoro anasema kuwa mapngao wa kilimo kwanza umezinduliwa bila kuwaeleza wananchi jinsi ya kupoata taarifa na fursa za kilimo. Wanaopata ni wawekezaji pekee.amesmea neon mapinduzi ya kijani ni neno ngumu ambalo sii kila mkulima anaweza kulizungumzia. “ Kilimo kwanza ni mpango wa kuwafukuza wakulima wadogo masikini kutoka kwenye ardhi yao na kuwapatia wageni, kwani kwa miaka ya hivi karibuni inaonekana kuwa migogoro ya ardhi inaongezeka.

Tamasha la Jinsia litujenge kudai haki ya kumiliki ardhi

Tamasha la Jinsia litujenge kudai haki ya kumiliki ardhi na demokrasia shirikishi
Na Deogratius Temba
ARDHI ni rasilimali na muhimili muhimu katika maisha ya wanadamu. Ardhi ya Tanzania ni mali yetu na ni lazima tuilinde na kuipigania. Kama kuna changamoto kubwa kwa jamii ya kitanzania katika kipindi hiki cha mfumo wa soko huria na kukua kwa utandawazi ni kukosekana kabisa kwa haki ya raia ya kumiliki ardhi, kuongezeka kwa migogoro ya ardhi ambayo ni matokeo ya kukua kwa soko huria.
Kilio kikubwa sasa ni uporaji wa ardhi kutokana na kuongezeka kwa kasi ya uwekezaji kwenye sekta ya kilimo.
Uporaji wa ardhi ni adui wa usawa wa kijinsia, soko huria halina huruma wala ubindamu lengo lake ni kuongeza faida na mali. Sheria za ardhi tulizojitungia zimetamka bayana usawa wa kijinsia lakini hatuzifuati kutokana na kusukumwa na mfumo huu kandamizi.
Sheria zimeeleza wazi juu ya ugawaji wa ardhi na haki ya kila binadamu bila kubagua. Sheria hizi ni kama :Sheria ya Ardhi namba 4 ya 1999, Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999. Sheria ya Mahakama za Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi namba 2 ya 2002, na Marekebisho ya sheria ya Ardhi namba 2 ya 2004.
Sheria nyingine muhimu ni Sheria ya Mahakama za utatuzi wa migogoro ya ardhi ilipitishwa mwaka 2002 na kuanza kutumika rasmi mwezi Oktoba 2003.
Pamoja na changamoto ya udhaifu wa sheria hizi, ambazo baadhi ya vipengele havimpi fursa mwananchi masikini hasa yule aliyeko pembezoni.
Ni lazima tukuabali na kuamini kuwa raia wote wanawake na wanaume wana haki sawa ya kupata, kumiliki, kutumia na kugawa ardhi. Milki za ardhi zilizopo ikiwa ni pamoja na milki za kimila zinatambuliwa na kulindwa kisheria bila kubagua jinsia.
Ardhi itumike kwa manufaa yanayozingatia maendeleo endelevu, fidia kamili na ya haki ilipwe kwa mmilika bila kuchelewa pale ardhi yake serikali ina poitwaa kwa manufaa ya umma, na manufaa ya umma yasiwe ni kumpa mwekezaji bali ni huduma za kajamii ambazo zitamnufaisha mwananchi masikini anayeishi katika eneo husika.
Serikali inapaswa kuweka mfumo bora wa utawala na usimamizi wa ardhi ambao unawawezesha wananchi kushiriki katika kufanya maamuzi kuhusu masuala ya ardhi wanayokalia au kutumia.
Sheria hizi zinatamka bayana kuwa mwanamke ana haki sawa na mwanaume katika kupata, kumiliki, kutumia na kugawa ardhi. Kifungu 3(2) cha sheria ya ardhi na sheria ya ardhi ya vijiji za 1999. Leo hii taifa linakumbwa na changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi ambapo tumefikia hatua ya uvunjifu wa amani na hadi umwagaji damu na pengine vifo kutokea katika maeneo kadhaa.
Hali hii imeondoa utamaduni wetu wa asili wa kuvumiliana na kumaliza matatizo yetu kwa njia mwafaka za mazungumzo. Ni muhimu serikali ikaelewa kwamba kupuuza migogoro hii ya ardhi nchini ni sawa na kuatamia bomu, hivyo ni lazima hatua za haraka zichukuliwe!
Migogoro, hasa ya wananchi na wawekezaji inakua kwa kasi na kuchukua sura mpya. Anapokuja ‘mgeni’, kwa jina la ‘Mwekezaji’ matendo ya Serikali yetu, yanapingana na usemi usemao ‘mgeni njoo mwenyeji apone’ bali imekuwa ‘mgeni njoo mwenyeji asulubike’ .tunahitaji umakini mkubwa katika kusimamia rasilimali ardhi bila kubagua na kuwanyanyasa wananchi wazawa.
Migogoro huu imesababishwa na tatizo kuwa la kukosekana kwa demokrasia shirikishi ambayo inampa kila mwananchi, mwanajamii fursa ya kuhoji, kuuliza na kusema juu ya rasilimali zinazomzunguka.
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na mtandao wa mashirika watetezi wa haki za binadamu,usawa wa kijinsia na ukombozi wa wanawake nchini (FemAct) na washirika wengine, wanaandaa Tamasha la Jinsia litalofanyika mwezi huu wa Septemba katika viwanja vya TGNP Mabibo Dar es salaam.
Mratibu wa tamasha hilo, Eluka Kibona, anasema kuwa tamasha hilo litafanyika kwa siku tatu kuanzia Septemba 13 hadi 16 mwaka huu.
Malengo ya tamasha hilo la kumi ambalo hufanyika kila baada ya miaka miwili kuwa ni kuibua, kubadilishana na kuanzisha fikra, uchambuzi wa kutengeneza mikakati ya pamoja ya kudai rasilimali ziwanufaishe wanawake, wanaume na vijana walioko pembezoni.
Kusherekea nguvu zetu za pamoja, kupanua na kuimarisha ushirikiano katika vuguvugu la ukombozi wa wanawake kimapinduzi na haki ya uchumi katika ngazi ya sekta zote za kijamii na mengineyo.
Muktadha wa tamasha la mwaka huu kwa mujibu wa FemAct ni kulenga kwenye matamasha ya awali na kujikita katika kuendeleza kampeni kubwa ya haki ya uchumi: ‘Rasilimali ziwanufaishe wanawake walioko pembezoni’.
Pia ni kuimarisha mapambano dhidi ya mfumo dume, sera za kibeberu na mifumo ya utandawazi wakati huu muafaka wa uundaji wa katiba mpya na kusherehekea mika 50 baada ya uhuru wa Tanzania.
Mada kuu ya tamasha ni Jinsia, Demokrasia na Maendeleo: Ardhi, Ajira na Maisha Endelevu. Lakini vile vile kutakuwa na mada ndogo zitakazotolewa kila siku. Na washiriki ni watu binafsi,vikundi,mashirika,taasisi mbalimbali na mitandao iliyoko katika mapambano yanafanana.
Kupitia tamasha hili, sote tutapata fursa ya kukaa pamoja na kudajali changamoto za ardhi, maji, masoko, biashara, ajira, na demokrasia katika taifa letu. Uchambuzi huu utatuapa nafasi ya kupaaza sauti zetu na kudai kile tulichoporwa. Tuungane pamoja!!